-
Kamusi Elezi ya Kiswahili (JKF) by JKF
Kamusi Elezi ye Kiswahili ni kamusi ya kisasa iliyoandikwa kwa ufindi wa kipekee na iliyo na maelezo ya vidahizo, Na kamusi iliyofungamana na hatua za kimaendeleo katika taaluma ya lugha ya Kiswahili na fasihi yake Itawafaa wataalamu, wanafunzi na walumizi wengine wa lugha ya Kiswahili. NI kamusi yenye upeo wa kimataifa. Licha ya maneno, semi na maelezo yake, ina vielezo vya michoro na matamshi ya vidahizo
Site kuu za Kamusi Elezi ya Kiswahlli • Vidahizo vipatavyo 45,000 • Maneno mapya yapatayo I.000 • Jopo la wataalamu wenye tajiriba kutoka Kenya. Tanzania na Japani • Matamshi murua kifonetiki: kulingana na alfabeti ya kifonetiki ya kimataifa • maelezo kamilifu ya kidahizo bila kutengemea visawe• Ufafanuzi wa kipekee wa methali, misemo na nahau • Kuhusishwa kwa dhana mpya za teknolopa na sayansi • msamiati mpya wa samaki na vyombo vya bahari • Mifano mwalaka yenye kushadidia maana • michoro na picha maridhawa zinazooana na maelezo
-
Kamusi ya Visawe by EAEP
Kamusi ya Visawe
Swahili Dictionary of Synonyms
Kamusi ya Visawe ni kamusi ya kwanza kushughulikiwa na kuchapishwa katika Kiswahili kwa madhumuni ya kutoa tafsiri ya neno fulani kwa kupata neno ama maneno mengine yenye maana halisi au yenye maana halisi au yenye maana ya karibu na neno linalotafsiriwa.
Kamusi hii imekusanya vidahizo visivyopungua 14,000 vingine vikiwa na visawe vine na zaidi. Kamusi hii pia imejaribu kuonyesha hall tofauti tofauti za vidahizo kama vile vitenzi au jina. Kwa hivyo, ni wazi kuwa lugha ya Kiswahili imejaa utajiri mwingi wa msamiati na mtumiaji yeyote wa lugha hii, anayetumia Kamusi ya visawe, hana haja ya kutapatapa kujieleza kwani atakuwa amesheheni maneno tele yenye maana moja.
Kamusi hii ni akiba kubwa yenye manufaa mengi hasa kwa wanafunzi wa shule za msingi, shule za upili, Vyuo Vikuu na pia kwa walimu na wanafunzi wa lugha ya Kiswahili popote pengine.
Mohammed Abdulla Mohamed alizaliwa Zanzibar na kusomea huko huko. Alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salamu na kupata shahada ya BA Hons na MA katika Elimu. Baadaye alijiunga na Chuo kikuu cha Columbia ambapo alipata shahada ya Ph.d katika isimu ya kufundisha. Alipata shahada ya MSc (Hons) katika Chuo Kikuu cha New York baadaye. Pia amewahi kuwa mhadhiri katika vyuo mbalimbali nchini Tanzania na Kenya.
Said A. Mohamed alizaliwa Ugunja mwaka wa 1947. Alisomea huko huko na kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Kisha Chuo Kikuu cha Leipzig, Ujerumani. Amefundisha katika shule za upili na Vyuo mbalimbali.
Usanifu wa jalada: Adrian Kheri Yongo
East African Educational Publishers Ltd
Nairobi. Kampala .Dar es Salaam • Kigali
Kamusl ya Vlsawe
Shop By Categories
- International Curriculum
- Marketplace – Used Books!
- National Curriculum
- TVET/Higher Learning
- Lab Equipment
- General Books
- International Curriculum
- Marketplace – Used Books!
- National Curriculum
- TVET/Higher Learning
- Lab Equipment
- General Books